< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
Dāvida dziesma. Dziedātāju vadonim pēc: „rīta blāzmas stirna“. Mans Dievs! Mans Dievs! Kāpēc Tu mani esi atstājis? Tu esi tālu no manas palīdzības, no manas kaukšanas vārdiem.
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
Mans Dievs, es saucu dienā, bet Tu man neatbildi, un nakti es arī klusu neciešu.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
Bet Tu esi svēts, dzīvodams starp Israēla slavas dziesmām.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
Uz Tevi mūsu tēvi cerējuši, tie ir cerējuši, un Tu tos esi izglābis.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
Uz Tevi tie saukuši un ir izpestīti, tie cerējuši uz Tevi un nav palikuši kaunā.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
Bet es esmu tārps un ne cilvēks, cilvēku apsmiekls un ļaužu nicināts.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
Visi, kas mani redz, mani apmēda, atplēš lūpas un krata galvu sacīdami:
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
Viņš to Tam Kungam sūdzējis; lai Tas viņu izrauj un viņu izglābj, ja Tam pie viņa ir labs prāts.
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
Tomēr Tu tas esi, kas mani izvedis no mātes miesām; Tu man licis paļauties uz Tevi no mātes krūtīm.
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
Uz Tevi es esmu mests no mātes klēpja, no mātes miesām Tu esi mans Dievs.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Neesi tālu no manis, jo bailība ir tuvu, jo palīga nav.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Lieli vērši mani apstājuši, trekni buļļi ap mani apmetušies.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
Tie atplēš savu rīkli pret mani kā lauva, plezdams un rūkdams.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
Es esmu izgāzts kā ūdens, visi mani kauli ir izlauzti, mana sirds ir manās miesās kā izkausēts vasks.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
Mans spēks ir izkaltis kā poda gabals, un mana mēle līp pie mana zoda, un Tu mani nolieci nāves pīšļos,
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
Jo suņi mani apstājuši, un ļaundarītāju bars ap mani ir apmeties, tie manas rokas un manas kājas ir izurbuši.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
Es visus savus kaulus varu skaitīt, bet viņi skatās un lūko uz mani ar prieku.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
Tie dala manas drēbes savā starpā un met kauliņus par manu apģērbu.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
Bet Tu, ak Kungs, neesi tālu, mans stiprums, steidzies man palīgā.
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Izglāb manu dvēseli no zobena, manu vientuli no suņu varas.
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Izpestī mani no lauvas rīkles un paklausi mani no vēršu ragiem.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
Es sludināšu Tavu vārdu saviem brāļiem, es Tevi slavēšu draudzes vidū.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
Slavējiet To Kungu, jūs, kas Viņu bīstaties, viss Jēkaba dzimums lai Viņu godā, un bīstaties, viss Israēla dzimums.
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
Jo Viņš nav nicinājis nedz apsmējis bēdīga bēdas, nedz no tā apslēpis Savu vaigu, un kad tas Viņu piesauca, tad Viņš paklausīja.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
No Tevis es dziedāšu tai lielā draudzē, es maksāšu savus solījumus to priekšā, kas Viņu bīstas.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
Tie bēdīgie ēdīs un būs paēduši, un kas To Kungu meklē, Viņu slavēs; jūsu sirds dzīvos mūžīgi.
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
Visi zemes gali to pieminēs un atgriezīsies pie Tā Kunga, un visas pagānu tautas klanīsies Viņa priekšā.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
Jo Tam Kungam pieder tā valstība, un Viņš valda pār tām tautām.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
Visi treknie virs zemes ēdīs un pielūgs, visi, kas pīšļos guļ, klanīsies Viņa priekšā, arī tie, kas nevarēja uzturēt savu dzīvību.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
Viņam būs dzimums, kas Viņam kalpos, par To Kungu sludinās līdz radu radiem;
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
Nāks un sludinās Viņa taisnību tiem ļaudīm, kas vēl dzims, ka Viņš to ir darījis.

< Zaburi 22 >