< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
My God, my God, why have you forsaken me? Why are you so far from yishu'ah ·delivering· me, and from the words of my groaning?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
My God, I cry in the daytime, but you don’t answer; in the night season, and am not silent.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
But you are holy, you who inhabit the tehilahot ·praise songs· of Israel [God prevails].
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
Our fathers trusted in you. They trusted, and you delivered them.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
They cried to you, and were delivered. They trusted in you, and were not disappointed.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised by the people.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
All who see me jeer at me. They insult me and shake their heads:
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
“He trusts in Adonai; so let him set him free! Let him rescue him, since he delights in him.”
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
But you brought me out of the womb. You made me trust while at my mother’s breasts.
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
I was thrown on you from my mother’s womb. You are my God since my mother bore me.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Don’t be far from me, for trouble is near. For there is no one to help.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Many bulls have surrounded me. Strong bulls of Bashan have encircled me.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
They open their mouths wide against me, lions tearing prey and roaring.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
I am poured out like water. All my bones are out of joint. My heart is like wax; it is melted within me.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
My strength is dried up like a potsherd. My tongue sticks to the roof of my mouth. You have brought me into the dust of death.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have surrounded me. A company of villains have enclosed me. They have pierced my hands and feet.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
I can count all of my bones. They look and stare at me.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They divide my garments among them. They cast lots for my clothing.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
But don’t be far off, Adonai. You are my help: hurry to help me.
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Deliver my soul from the sword, my precious life from the power of the dog.
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Save me from the lion’s mouth! Yes, from the horns of the wild oxen, you have answered me.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
I will declare your name to my brothers. Among the assembly, I will praise you.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
You who fear Adonai, praise him! All you descendants of Jacob [Supplanter], glorify him! Stand in awe of him, all you descendants of Israel [God prevails]!
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
For he has not despised nor abhorred the affliction of the afflicted, Neither has he hidden his face from him; but when he cried to him, he sh'ma ·heard obeyed·.
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
Of you comes my tehilah ·praise song· in the great assembly. I will pay my vows before those who fear him.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
The humble shall eat and be satisfied. They shall praise Adonai who seek after him. Let your hearts live forever.
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
All the ends of the earth shall remember and turn to Adonai. All the relatives of the nations shall hawa ·bow low, prostrate· to worship before you.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
For the kingdom is Adonai’s. He is the ruler over the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
All the rich ones of the earth shall eat and worship. All those who go down to the dust shall bow before him, even he who can’t keep his soul alive.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
Posterity shall serve him. Future generations shall be told about the Lord.
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
They shall come and shall declare his righteousness to a people that shall be born, for he has done it.

< Zaburi 22 >