< Zaburi 20 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mungu akusaidie wakati wa shida; na jina la Mungu wa Yakobo likulinde
May Adonai answer you in the day of trouble. May the name of the God of Jacob [Supplanter] set you up on high,
2 na kutuma msaada kutoka mahali patakatifu kwa ajili ya kukutegemeza wewe kutoka Sayuni.
send you help from the sanctuary, grant you support from Zion [Mountain ridge, Marking],
3 Naye akumbuke sadaka yako yote na kuipokea sadaka ya kuteketezwa.
remember all your offerings, and accept your burned sacrifice. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
4 Naye akujalie haja za moyo wako na kutimiza mipango yako yote.
May He grant you your heart’s desire, and fulfill all your counsel.
5 Ndipo tutakapo shangilia katika ushindi wako, na, katika jina la Mungu wetu, tutapeperusha bendera. Yahwe naakupe maombi yako yote ya haki.
We will triumph in your yishu'ah ·salvation·. In the name of our God, we will set up our banners. May Adonai grant all your requests.
6 Sasa ninajua ya kuwa Yahwe atawaokoa wapakwa mafuta wake; yeye atamjibu yeye kutoka katika mbingu takatifu kwa uweza wa mkono wake wa kuume ambao waweza kumuokoa yeye.
Now I know that Adonai saves his anointed. He will answer him from his holy heaven, with the yesha' ·saving· strength of his right hand.
7 Baadhi hamini katika magari na wengine katika farasi, lakini sisi tumuita Yahwe Mungu wetu.
Some trust in chariots, and some in horses, but we trust the name of Yahweh Eloheikhem [Yahweh our God].
8 Wao watashushwa chini na kuanguka, bali sisi tutainuka na kusimama wima!
They are bowed down and fallen, but we rise up, and stand upright.
9 Yahwe, umuokoe mfalme; utusaidie sisi tukuitapo.
Save, Adonai! Let the King answer us when we call!

< Zaburi 20 >