< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
¿Para qué están en tumulto las naciones, Y los pueblos maquinan cosas vanas?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
Los reyes de la tierra se levantarán, Y gobernantes conspirarán unidos Contra Yavé y contra su Ungido, y dicen:
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
¡Rompamos sus ataduras Y quitemos de nosotros sus cuerdas!
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
El que está sentado en los cielos se reirá. ʼAdonay se burlará de ellos.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Luego les hablará en su furor. Los conturbará en su ira.
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Yo mismo consagré a mi Rey sobre Sion, Mi Montaña Santa.
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
Yo promulgaré el decreto. Yavé me dijo: Mi Hijo eres Tú, Yo te engendré hoy.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Pídeme y te daré los pueblos en posesión, Y como herencia tuya los confines de la tierra.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
Los quebrantarás con vara de hierro. Los harás añicos como vasija de alfarero.
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
Ahora pues, oh reyes, actúen con sabiduría. Acepten amonestación, jueces de la tierra:
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Sirvan a Yavé con temor Y regocíjense con temblor.
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Besen los pies al Hijo No sea que se enoje y perezcan en el camino, Pues de repente arde su ira. Inmensamente felices son los que se refugian en Él.

< Zaburi 2 >