< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Why? do they plot nations and peoples do they devise? vanity.
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
They take their stand - [the] kings of [the] earth and rulers they seat themselves together on Yahweh and on anointed his.
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
Let us tear off fetters their and let us throw away from us ropes their.
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
[the one who] sits In the heavens he laughs [the] Lord he mocks them.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Then he speaks to them in anger his and in fury his he terrifies them.
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
And I I have installed king my on Zion [the] mountain of holiness my.
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
I will recount concerning [the] decree of Yahweh he said to me [are] son my you I this day I have begotten you.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Ask from me so let me make nations inheritance your and possession your [the] ends of [the] earth.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
You will break them with a rod of iron like a vessel of a potter you will smash them.
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
And therefore O kings act prudently let yourselves be instructed O rulers of [the] earth.
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Serve Yahweh with fear and rejoice with trembling.
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Kiss [the] son lest he should be angry - and you may perish way if it burns like a little anger his how blessed! [are] all [those who] seek refuge in him.

< Zaburi 2 >