< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
Psalm: Oratio David. Exaudi Domine iustitiam meam: intende deprecationem meam. Auribus percipe orationem meam, non in labiis dolosis.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
De vultu tuo iudicium meum prodeat: oculi tui videant aequitates.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Probasti cor meum, et visitasti nocte: igne me examinasti, et non est inventa in me iniquitas.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
Ut non loquatur os meum opera hominum: propter verba labiorum tuorum ego custodivi vias duras.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
Perfice gressus meos in semitis tuis: ut non moveantur vestigia mea.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
Ego clamavi, quoniam exaudisti me Deus: inclina aurem tuam mihi, et exaudi verba mea.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Mirifica misericordias tuas, qui salvos facis sperantes in te.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
A resistentibus dexterae tuae custodi me, ut pupillam oculi. Sub umbra alarum tuarum protege me:
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
a facie impiorum qui me afflixerunt. Inimici mei animam meam circumdederunt,
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
adipem suum concluserunt: os eorum locutum est superbiam.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
Proiicientes me nunc circumdederunt me: oculos suos statuerunt declinare in terram.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
Susceperunt me sicut leo paratus ad praedam: et sic catulus leonis habitans in abditis.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Exurge Domine, praeveni eum, et supplanta eum: eripe animam meam ab impio, frameam tuam
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
ab inimicis manus tuae. Domine a paucis de terra divide eos in vita eorum: de absconditis tuis adimpletus est venter eorum. Saturati sunt filiis: et dimiserunt reliquias suas parvulis suis.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
Ego autem in iustitia apparebo conspectui tuo: satiabor cum apparuerit gloria tua.

< Zaburi 17 >