< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
A prayer of David. Listen to my plea for justice, Yahweh; pay attention to my call for help! Give ear to my prayer from lips without deceit.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Let my vindication come from your presence; let your eyes see what is right!
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
If you test my heart, if you come to me in the night, you will purify me and will not find any evil plans; my mouth will not transgress.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
As for the deeds of mankind, it is at the word of your lips that I have kept myself from the ways of the lawless.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
My steps have held firmly to your tracks; my feet have not slipped.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
I call to you, for you answer me, God; turn your ear to me and listen when I speak.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Show your covenant faithfulness in a wonderful way, you who save by your right hand those who take refuge in you from their enemies!
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Protect me like the apple of your eye; hide me under the shadow of your wings
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
from the presence of the wicked ones who assault me, my enemies who surround me.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They have no mercy on anyone; their mouths speak with pride.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
They have surrounded my steps. They set their eyes to strike me to the ground.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
They are like a lion eager for a victim, like a young lion crouching in hidden places.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, Yahweh! Attack them! Throw them down on their faces! Rescue my life from the wicked by your sword!
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
Rescue me from men by your hand, Yahweh, from men of this world whose prosperity is in this life alone! You will fill the bellies of your treasured ones with riches; they will have many children and will leave their wealth to their children.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
As for me, I will see your face in righteousness; I will be satisfied, when I awake, with a sight of you.

< Zaburi 17 >