< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
A prayer of David. Listen, O Lord, to my innocence; attend to my piercing cry. Give heed to my prayer out of lips unfeigned.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Let my vindication come from you, your eyes see the truth.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
When you test my heart when you visit at night, and assay me like silver – you can find no evil. I am determined that my mouth should not lie.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
I gave earnest heed to the words of your lips.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
My steps have held fast to the paths of your precepts and in your tracks have my feet never stumbled.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
So I call you, O God, with assurance of answer; bend down your ear to me, hear what I say.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Show your marvelous love, you who save from enemies those who take refuge at your right hand.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye, hide me in the shelter of your wings.
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From wicked people who do me violence, from deadly foes who crowd around me.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They have closed their hearts to pity, the words of their mouths are haughty.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
Now they dog us at every step, keenly watching, to hurl us to the ground,
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
like a lion, longing to tear, like a young lion, lurking in secret.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, Lord, face them and fell them. By your sword set me free from the wicked,
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
by your hand, O Lord, from those – whose portion of life is but of this world. But let your treasured ones have food in plenty may their children be full and their children satisfied.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
In my innocence I will see your face, awake I am filled with a vision of you.

< Zaburi 17 >