< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
A PRAYER OF DAVID. Hear, O YHWH, righteousness, attend my cry, Give ear [to] my prayer, without lips of deceit.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
My judgment goes out from before You; Your eyes see uprightly.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
You have proved my heart, You have inspected by night, You have tried me, You find nothing; My thoughts do not pass over my mouth.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
As for doings of man, Through a word of Your lips I have observed The paths of a destroyer;
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
To uphold my goings in Your paths, My steps have not slipped.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
I called You, for You answer me, O God, incline Your ear to me, hear my speech.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Separate Your kindness wonderfully, O Savior of the confiding, By Your right hand, from withstanders.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple, the daughter of the eye; Hide me in the shadow of Your wings,
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From the face of the wicked who spoiled me, [From] my enemies in soul who go around against me.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They have closed up their fat, Their mouths have spoken with pride:
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
“Our steps have now surrounded [him]”; They set their eyes to turn aside in the land.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
His likeness as a lion desirous to tear, As a young lion dwelling in secret places.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, O YHWH, go before his face, Cause him to bend. Deliver my soul from the wicked, Your sword,
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
From men, Your hand, O YHWH, From men of the world, their portion [is] in life, And [with] Your hidden things You fill their belly, They are satisfied [with] sons, And have left their abundance to their sucklings.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
I—in righteousness, I see Your face; I am satisfied, in awaking, [with] Your form!

< Zaburi 17 >