< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
A Prayer of David. Hear the right, O LORD, attend unto my cry, give ear unto my prayer, [that goeth] not out of feigned lips.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Let my sentence come forth from thy presence; let thine eyes behold the things that are equal.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Thou hast proved mine heart; thou hast visited [me] in the night; thou hast tried me, [and] shalt find nothing; I am purposed [that] my mouth shall not transgress.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
Concerning the works of men, by the word of thy lips I have kept [me from] the paths of the destroyer.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
Hold up my goings in thy paths, [that] my footsteps slip not.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
I have called upon thee, for thou wilt hear me, O God: incline thine ear unto me, [ and hear] my speech.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Shew thy marvellous lovingkindness, O thou that savest by thy right hand them which put their trust [in thee] from those that rise up [against them].
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye, hide me under the shadow of thy wings,
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From the wicked that oppress me, [from] my deadly enemies, [who] compass me about.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
They are inclosed in their own fat: with their mouth they speak proudly.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
They have now compassed us in our steps: they have set their eyes bowing down to the earth;
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
Like as a lion [that] is greedy of his prey, and as it were a young lion lurking in secret places.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, O LORD, disappoint him, cast him down: deliver my soul from the wicked, [which is] thy sword:
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
From men [which are] thy hand, O LORD, from men of the world, [which have] their portion in [this] life, and whose belly thou fillest with thy hid [treasure: ] they are full of children, and leave the rest of their [substance] to their babes.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
As for me, I will behold thy face in righteousness: I shall be satisfied, when I awake, with thy likeness.

< Zaburi 17 >