< Zaburi 17 >

1 Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
A Prayer of David. Hear the right, O LORD, attend unto my cry; give ear unto my prayer from lips without deceit.
2 Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
Let my judgment come forth from Thy presence; let Thine eyes behold equity.
3 Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
Thou hast tried my heart, Thou hast visited it in the night; Thou hast tested me, and Thou findest not that I had a thought which should not pass my mouth.
4 Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
As for the doings of men, by the word of Thy lips I have kept me from the ways of the violent.
5 Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
My steps have held fast to Thy paths, my feet have not slipped.
6 Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
As for me, I call upon Thee, for Thou wilt answer me, O God; incline Thine ear unto me, hear my speech.
7 Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
Make passing great Thy mercies, O Thou that savest by Thy right hand from assailants them that take refuge in Thee.
8 Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye, hide me in the shadow of Thy wings,
9 kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
From the wicked that oppress, my deadly enemies, that compass me about.
10 Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
Their gross heart they have shut tight, with their mouth they speak proudly.
11 Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
At our every step they have now encompassed us; they set their eyes to cast us down to the earth.
12 Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
He is like a lion that is eager to tear in pieces, and like a young lion lurking in secret places.
13 Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
Arise, O LORD, confront him, cast him down; deliver my soul from the wicked, by Thy sword;
14 Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
From men, by Thy hand, O LORD, from men of the world, whose portion is in this life, and whose belly Thou fillest with Thy treasure; who have children in plenty, and leave their abundance to their babes.
15 Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.
As for me, I shall behold Thy face in righteousness; I shall be satisfied, when I awake, with Thy likeness.

< Zaburi 17 >