< Zaburi 149 >

1 Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
Praise ye Jah! Sing ye to Jehovah a new song, His praise in an assembly of saints.
2 Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
Israel doth rejoice in his Maker, Sons of Zion do joy in their king.
3 Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
They praise His name in a dance, With timbrel and harp sing praise to Him.
4 Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
For Jehovah is pleased with His people, He beautifieth the humble with salvation.
5 Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
Exult do saints in honour, They sing aloud on their beds.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
The exaltation of God [is] in their throat, And a two-edged sword in their hand.
7 kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
To do vengeance among nations, Punishments among the peoples.
8 Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
To bind their kings with chains, And their honoured ones with fetters of iron,
9 Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.
To do among them the judgment written, An honour it [is] for all his saints. Praise ye Jah!

< Zaburi 149 >