< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu. 2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote. 3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo. 4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga. 5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa. 6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika. 7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari, 8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake. 9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote, 10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege. 11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi, 12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto. 13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu. 14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< Zaburi 148 >