< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
Praise Yahweh. Praise Yahweh, you in the heavens; praise him, you in the heights.
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
Praise him, all his angels; praise him, all his hosts.
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
Praise him, sun and moon; praise him, all you shining stars.
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
Praise him, highest heaven and you waters that are above the sky.
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
Let them praise the name of Yahweh, for he gave the command, and they were created.
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
He has also established them forever and ever; he issued a decree that will never change.
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
Praise him from the earth, you sea monsters and all ocean depths,
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
fire and hail, snow and clouds, stormy wind fulfilling his word.
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
Praise him, mountains and all hills, fruit trees and all cedars,
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
animals wild and tame, creatures that crawl and birds.
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
Praise Yahweh, kings of the earth and all nations, princes and all who govern on the earth,
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
both young men and young women, elderly and children.
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
Let them all praise the name of Yahweh, for his name alone is exalted and his glory extends over the earth and the heavens.
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
He has lifted up the horn of his people for praise from all his faithful ones, the Israelites, the people near to him. Praise Yahweh.

< Zaburi 148 >