< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Hallelujah! Lobet den Namen Jehovahs, lobet, ihr Knechte Jehovahs!
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Ihr, die ihr steht in dem Hause Jehovahs, in den Höfen des Hauses unseres Gottes:
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Hallelujah; denn gut ist Jehovah. Singt Psalmen Seinem Namen; denn lieblich ist Er.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Denn Jakob hat Jah Sich erwählt, Israel zu Seinem besonderen Eigentum.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Denn ich weiß, daß groß ist Jehovah, und unser Herr vor allen Göttern;
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Alles, wozu Jehovah Lust hat, tut Er im Himmel und auf Erden, im Meer und allen Abgründen.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Er führt Dünste herauf vom Ende der Erde, macht Blitze zu Regen, bringt den Wind heraus aus Seinen Schätzen.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Der die Erstgeborenen Ägyptens schlug vom Menschen bis zum Vieh;
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Er sandte Zeichen und Wahrzeichen, in deine Mitte Ägypten, wider Pharao und wider alle seine Knechte.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Der viele Völkerschaften hat geschlagen und mächtige Könige erwürgte.
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sichon, den König der Amoriter, und Og, den König Baschans, und alle Königreiche Kanaans.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
Und Der ihr Land zum Erbe hat gegeben, zum Erbe Israel, Seinem Volke.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Jehovah, Dein Name ist ewig, Jehovah, Dein Gedächtnis zu Geschlecht und Geschlecht.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Denn Recht wird sprechen Seinem Volk Jehovah, und es wird Ihn gereuen wegen Seiner Knechte.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Die Götzen der Völkerschaften sind Silber und Gold, sie sind gemacht von den Händen des Menschen.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Einen Mund haben sie und reden nicht; Augen haben sie und sehen nicht.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Sie haben Ohren und nehmen nicht zu Ohren, auch ist in ihrem Mund kein Hauch.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Wie sie werden sein, die sie machen, ein jeder, der auf sie vertraut.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
O Haus Israel, segnet Jehovah; o Haus Aharons, segnet Jehovah!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
O Haus Levi, segnet Jehovah; die ihr Jehovah fürchtet, segnet Jehovah!
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Gesegnet sei Jehovah aus Zion, Er, Der in Jerusalem wohnt. Hallelujah!

< Zaburi 135 >