< Zaburi 128 >

1 Amebarikiwa kila mtu amchaye Yahwe, atembeaye katika njia zake. 2 Kazi ya mikono yako, wewe utaifurahia; utabarikiwa na kufanikiwa. 3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao katika nyumba yako; wanao watakuwa kama miche ya mimea ya mizeituni wakaapo kuzunguka meza yako. 4 Ndiyo, hakika, mtu anaye muheshimu Yahwe atabarikiwa. 5 Mungu na akubariki toka Sayuni; na uweze kuona mafanikio ya Yerusalemu siku zote za maisha yako. 6 Uishi uwaone wana wa wanao. Amani iwe na Israli.

< Zaburi 128 >