< Zaburi 125 >

1 Wale wamwaminio Yahwe ni kama mlima Sayuni, hautikisiki, wadumu milele.
Those who trust in Adonai are as Mount Zion [Mountain ridge, Marking], which can’t be moved, but remains forever.
2 Kama milima inavyo izunguka Yerusalemu, hivyo ndivyo Yahwe anavyo wazunguka watu wake sasa na hata milele.
As the mountains surround Jerusalem [City of peace], so Adonai surrounds his people from this time forward and forever more.
3 Fimbo ya uovu haitatawala katika nchi ya wenye haki. Vinginevyo wenye haki wanaweza kukosea.
For the scepter of wickedness won’t remain over the allotment of the upright; so that the upright won’t use their hands to do evil.
4 Ee Yahwe, utende wema kwa wale walio wema na wale walio wanyoofu mioyoni mwao.
Do good, Adonai, to those who are good, to those who are upright in their hearts.
5 Lakini kwa wale wanaogeukia njia zao za upotovu, Yahwe atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani iwe na Israeli.
But as for those who turn aside to their crooked ways, Adonai will lead them away with the workers of iniquity. Peace be on Israel [God prevails].

< Zaburi 125 >