< Zaburi 120 >

1 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
A Song of the Ascents. Unto Jehovah in my distress I have called, And He answereth me.
2 Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
O Jehovah, deliver my soul from a lying lip, From a deceitful tongue!
3 Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
What doth He give to thee? And what doth He add to thee? O deceitful tongue!
4 Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
Sharp arrows of a mighty one, with broom-coals.
5 Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
Woe to me, for I have inhabited Mesech, I have dwelt with tents of Kedar.
6 Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
Too much hath my soul dwelt with him who is hating peace.
7 Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.
I [am] peace, and when I speak they [are] for war!

< Zaburi 120 >