< Zaburi 118 >

1 Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Aleluja! Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!
2 Israeli na aseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
Neka rekne dom Izraelov: “Vječna je ljubav njegova!”
3 Nyumba ya Haruni na iseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
Neka rekne dom Aronov: “Vječna je ljubav njegova!”
4 Wafuasi waaminifu wa Yahwe na waseme, “Uaminifu wa agano lake wadumu milele.”
Svi koji se Jahve boje neka reknu: “Vječna je ljubav njegova!”
5 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe; Yahwe alinijibu na kuniweka huru.
Iz tjeskobe Jahvu ja zazvah: on me usliša i oslobodi.
6 Yahwe yuko pamoja nami; sitaogopa; mwanadamu atanifanya nini? Yahwe yuko upande wangu kama msaidizi;
Jahve je sa mnom i ja ne strahujem: što mi tko može?
7 nitawatazama kwa ushindi wale walio nichukia.
Jahve je sa mnom, pomoć moja, i zbunjene gledam dušmane.
8 Ni bora kuwa na makazi katika Yahwe kuliko kumtumainia mwanadamu.
Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u čovjeka.
9 Ni bora kukimbilia katika Yahwe kuliko kuamini katika wakuu.
Bolje se Jahvi uteći nego se uzdat' u mogućnike.
10 Mataifa yote walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
Pogani me okružiše: imenom ih Jahvinim uništih.
11 Walinizunguka; naam, walinizunguka; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
Opkoliše me odasvud: imenom ih Jahvinim uništih.
12 Walinizunguka kama nyuki; walitoweka haraka kama moto kati ya miiba; kwa jina la Yahwe niliwakatilia mbali.
Opkoliše me poput pčela, ubod im žeže kao trnje zapaljeno: imenom ih Jahvinim uništih.
13 Walinishambulia ili waniangushe, lakini Yahwe alinisaidia.
Gurahu me, gurahu, da me obore, ali mi Jahve pomože.
14 Yahwe ni nguvu yangu na furaha yangu, na ndiye anaye niokoa.
Jahve je moja snaga i pjesma, on mi je spasitelj.
15 Kelele za ushindi zimesikika katika maskani ya wenye haki; mkono wa kuume wa Mungu umeshinda.
Čuj! Radost i spasenje odzvanja šatorima pravednika: Jahvina se proslavi desnica,
16 Mkono wa kuume wa Mungu umetukuka; mkono wa kuume wa Yahwe umeshinda.
Jahvina me uzdigne desnica, Jahvina se proslavi desnica!
17 Sitakufa, bali nitaishi na kuyatangaza matendo ya Yahwe.
Ne, umrijeti neću nego živjeti i kazivat ću djela Jahvina.
18 Yahwe ameniadhibu vikali; lakini hajaruhusu nife.
Kaznom teškom kaznio me Jahve, ali me smrti ne preda.
19 Unifungulie milango ya haki; nitaingia na nitamshukuru Yahwe.
Otvorite mi širom vrata pravde: ući ću, Jahvi zahvalit'!
20 Hili ni lango la Yahwe; wenye haki hupitia kwalo.
“Ovo su vrata Jahvina, na njih ulaze pravedni!”
21 Nitakushukuru wewe, kwa kuwa ulinijibu, na umekuwa wokovu wangu.
Zahvalit ću ti što si me uslišio i moj postao spasitelj.
22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa wajenzi limekuwa msingi.
Kamen što ga odbaciše graditelji postade kamen zaglavni.
23 Yahwe ndiye afanyaye hili; ni la ajabu machoni petu.
Jahvino je to djelo: kakvo čudo u očima našim!
24 Hii ni siku ambayo Yahwe ametenda; tutaifurahia na kuishangilia.
Ovo je dan što ga učini Jahve: kličimo i radujmo se njemu!
25 Tafadhali, Yahwe, utupe ushindi! Tafadhali, Yahwe, utupe mafanikio!
O Jahve, spasenje nam daj! Jahve, sreću nam daj!
26 Amebarikiwa yule ajaye katika jina la Yahwe; tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yahwe.
Blagoslovljen koji dolazi u imenu Jahvinu! Blagoslivljamo vas iz Doma Jahvina!
27 Yahwe ni Mungu, na ametupa sisi nuru; ifungeni dhabihu kwa kamba pembeni mwa madhabahu.
Obasjao nas Bog Jahve! Složite povorku s grančicama u ruci sve do rogova žrtvenika.
28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakushukuru; wewe ni Mungu wangu; nitakutukuza wewe.
Ti si Bog moj - tebi zahvaljujem: Bože moj, tebe ja uzvisujem.
29 Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema; kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Zahvaljujte Jahvi jer je dobar, jer je vječna ljubav njegova!

< Zaburi 118 >