< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
Alleluia. In exitu Israel de Ægypto, domus Iacob de populo barbaro:
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
Facta est Iudæa sanctificatio eius, Israel potestas eius.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
Mare vidit, et fugit: Iordanis conversus est retrorsum.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
Montes exultaverunt ut arietes: et colles sicut agni ovium.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
Quid est tibi mare quod fugisti: et tu Iordanis, quia conversus es retrorsum?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
Montes exultastis sicut arietes, et colles sicut agni ovium?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
A facie Domini mota est terra, a facie Dei Iacob.
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
Qui convertit petram in stagna aquarum, et rupem in fontes aquarum.

< Zaburi 114 >