< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
When Israel left Egypt, the house of Jacob from a people who spoke a foreign language,
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
Judah became his holy place, Israel his kingdom.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
The sea looked and fled; the Jordan turned back.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, the hills skipped like lambs.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
Why did you flee, sea? Jordan, why did you turn back?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
Mountains, why did you skip like rams? You little hills, why did you skip like lambs?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
Tremble, earth, before the Lord, at the presence of the God of Jacob.
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
He turned the rock into a pool of water, the hard rock into a spring of water.

< Zaburi 114 >