< Zaburi 113 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Praise ye Jah! Praise, ye servants of Jehovah. Praise the name of Jehovah.
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
The name of Jehovah is blessed, From henceforth, and unto the age.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
From the rising of the sun unto its going in, Praised [is] the name of Jehovah.
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
High above all nations [is] Jehovah, Above the heavens [is] his honour.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who [is] as Jehovah our God, He is exalting [Himself] to sit?
6 atazamaye chini angani na duniani?
He is humbling [Himself] to look On the heavens and on the earth.
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
He is raising up from the dust the poor, From a dunghill He exalteth the needy.
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
To cause to sit with princes, With the princes of His people.
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
Causing the barren one of the house to sit, A joyful mother of sons; praise ye Jah!

< Zaburi 113 >