< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Alleluia. Confitebor tibi Domine in toto corde meo: in consilio iustorum, et congregatione.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Magna opera Domini: exquisita in omnes voluntates eius.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Confessio et magnificentia opus eius: et iustitia eius manet in sæculum sæculi.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Memoriam fecit mirabilium suorum, misericors et miserator Dominus:
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
escam dedit timentibus se. Memor erit in sæculum testamenti sui:
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
virtutem operum suorum annunciabit populo suo:
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
Ut det illis hereditatem gentium: opera manuum eius veritas, et iudicium.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
Fidelia omnia mandata eius: confirmata in sæculum sæculi, facta in veritate et æquitate.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Redemptionem misit populo suo: mandavit in æternum testamentum suum. Sanctum, et terribile nomen eius:
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
initium sapientiæ timor Domini. Intellectus bonus omnibus facientibus eum: laudatio eius manet in sæculum sæculi.

< Zaburi 111 >