< Zaburi 11 >

1 Ni kwako Yahweh ninapata usalama; ni kwa namna gani utasema na mimi, “Ruka kama ndege hadi mlimani”?
To the choirmaster of David in Yahweh - I have taken refuge how? will you say to self my (take flight *Qk) mountain your a bird.
2 Tazama! Waovu wana andaa pinde zao. Wana tayarisha gizani mishale yao kwenye kamba ili kufyatua mioyo ya wenye haki.
For there! the wicked they bend! a bow they have prepared arrow their on [the] string to shoot in darkness to [people] upright of heart.
3 Ikiwa misingi imeharibiwa, mwenye haki atafanya nini?
If the foundations they will be torn down! [the] righteous what? does he do.
4 Yahweh yuko katika hekalu takatifu; macho yake yanatazama, yakiuchunguza ubinadamu.
Yahweh - [is] in [the] temple of holiness his Yahweh [is] in the heavens throne his eyes his they see eyelids his they test [the] children of humankind.
5 Yahweh huwachunguza wote wenye haki na waovu, bali huwachukia wapendao kuwaumiza wengine.
Yahweh [the] righteous he tests and [the] wicked and [one who] loves violence it hates self his.
6 Yeye huwanyeshea waovu makaa ya mawe na moto wa jehanamu; upepo uunguzao utakuwa ni sehemu yao kutoka katika kikombe chake!
He will rain down on wicked [people] snares fire and sulfur and [will be] a wind of burning heat [the] portion of cup their.
7 Kwa kuwa Yahweh ni mwenye haki, Naye hupenda haki; wenye haki watauona uso wake.
For [is] righteous Yahweh righteousness he loves [the] upright they will see faces their.

< Zaburi 11 >