< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
To the choirmaster of David a psalm O God of praise my may not you be silent.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
For [the] mouth of [the] wicked and a mouth of deceit on me they have opened they have spoken with me a tongue of falsehood.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
And words of hatred they have surrounded me and they have fought against me without cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
In place of love my they accuse me and I [am] prayer.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
And they have put on me evil in place of good and hatred in place of love my.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Appoint on him a wicked [person] and an accuser let him stand on right [hand] his.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
When is judged he let him come forth guilty and prayer his let it become sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
May they be days his few office his may he take another.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
May they be children his fatherless ones and wife his a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
And really may they wander children his and they will beg and they will seek away from ruins their.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
May he strike a creditor to all that [belongs] to him and may they plunder strangers property his.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
May not it belong to him [one who] prolongs loyalty and may not it belong [one who] shows favor to fatherless children his.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
May it be posterity his to cut off in a generation another may it be wiped out name their.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
May it be remembered - [the] iniquity of ancestors his to Yahweh and [the] sin of mother his may not it be wiped out.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Let them be before Yahweh continually and may he cut off from [the] earth memory their.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Because that - not he remembered to do loyalty and he harassed anyone poor and needy and disheartened of heart to put to [them] death.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
And he loved a curse and it came to him and not he delighted in blessing and it was far from him.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
And he put on a curse like garment his and it went like water in inward part[s] his and like oil in bones his.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
May it be for him like a garment [which] he wraps himself and to a waistband [which] continually he girds on it.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
This [be] [the] wage[s] of accusers my from with Yahweh and those [who] speak evil on self my.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
And you - O Yahweh O Lord deal with me for [the] sake of name your for [is] good covenant loyalty your deliver me.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
For [am] poor and needy I and heart my someone has pierced in inner being my.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Like a shadow when stretches out it I have vanished I have been shaken off like locust.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Knees my they have staggered from fasting and flesh my it has become lean from fatness.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
And I - I have become a reproach to them they see me they shake! head their.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me O Yahweh God my save me according to covenant loyalty your.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
So they may know that [is] hand your this you O Yahweh you have done it.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
They will curse they and you you will bless they have arisen - and they have been ashamed and servant your he will rejoice.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
May they be clothed accusers my ignominy and may they be wrapped like robe shame their.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
I will give thanks to Yahweh exceedingly with mouth my and in among many [people] I will praise him.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
For he stands to [the] right [hand] of [the] needy to save [him] from [those who] judge self his.

< Zaburi 109 >