< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A Song, a Psalm of David. Prepared is my heart, O God, I sing, yea, I sing praise, also my honour.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, psaltery and harp, I awake the dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I thank Thee among peoples, O Jehovah, And I praise Thee among the nations.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For great above the heavens [is] Thy kindness, And unto the clouds Thy truth.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be Thou exalted above the heavens, O God, And above all the earth Thy honour.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That Thy beloved ones may be delivered, Save [with] Thy right hand, and answer us.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God hath spoken in His holiness: I exult, I apportion Shechem, And the valley of Succoth I measure,
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Mine [is] Gilead, mine [is] Manasseh, And Ephraim [is] the strength of my head, Judah [is] my lawgiver,
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab [is] a pot for my washing, Upon Edom I cast my shoe, Over Philistia I shout habitually.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who doth bring me in to the fenced city? Who hath led me unto Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Hast not Thou, O God, cast us off? And Thou goest not out, O God, with our hosts!
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give to us help from adversity, And vain is the salvation of man.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
In God we do mightily, And He doth tread down our adversaries!

< Zaburi 108 >