< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A Song, a Psalm of David. My heart is steadfast, O God; I will sing, yea, I will sing praises, even with my glory.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, psaltery and harp; I will awake the dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will give thanks unto Thee, O LORD, among the peoples; and I will sing praises unto Thee among the nations.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For Thy mercy is great above the heavens, and Thy truth reacheth unto the skies.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be Thou exalted, O God, above the heavens; and Thy glory be above all the earth.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That Thy beloved may be delivered, save with Thy right hand, and answer me.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God spoke in His holiness, that I would exult; that I would divide Shechem, and mete out the valley of Succoth.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine, Manasseh is mine; Ephraim also is the defence of my head; Judah is my sceptre.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab is my washpot; upon Edom do I cast my shoe; over Philistia do I cry aloud.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me into the fortified city? Who will lead me unto Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Hast not Thou cast us off, O God? and Thou goest not forth, O God, with our hosts?
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us help against the adversary; for vain is the help of man.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Through God we shall do valiantly; for He it is that will tread down our adversaries.

< Zaburi 108 >