< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alleluia. Confitemini Domino quoniam bonus: quoniam in sæculum misericordia eius.
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Dicant qui redempti sunt a Domino, quos redemit de manu inimici: et de regionibus congregavit eos:
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
A solis ortu, et occasu: ab Aquilone, et mari.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Erraverunt in solitudine in inaquoso: viam civitatis habitaculi non invenerunt,
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Esurientes, et sitientes: anima eorum in ipsis defecit.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum eripuit eos.
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
Et deduxit eos in viam rectam: ut irent in civitatem habitationis.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Confiteantur Domino misericordiæ eius: et mirabilia eius filiis hominum.
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
Quia satiavit animam inanem: et animam esurientem satiavit bonis.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Sedentes in tenebris, et umbra mortis: vinctos in mendicitate, et ferro.
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
Quia exacerbaverunt eloquia Dei: et consilium Altissimi irritaverunt.
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Et humiliatum est in laboribus cor eorum: infirmati sunt, nec fuit qui adiuvaret.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
Et eduxit eos de tenebris, et umbra mortis: et vincula eorum dirupit.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Confiteantur Domino misericordiæ eius: et mirabilia eius filiis hominum.
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Quia contrivit portas æreas: et vectes ferreos confregit.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Suscepit eos de via iniquitatis eorum: propter iniustitias enim suas humiliati sunt.
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Omnem escam abominata est anima eorum: et appropinquaverunt usque ad portas mortis.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Misit verbum suum, et sanavit eos: et eripuit eos de interitionibus eorum.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Confiteantur Domino misericordiæ eius: et mirabilia eius filiis hominum.
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Et sacrificent sacrificium laudis: et annuncient opera eius in exultatione.
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Qui descendunt mare in navibus, facientes operationem in aquis multis.
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
Ipsi viderunt opera Domini, et mirabilia eius in profundo.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
Dixit, et stetit spiritus procellæ: et exaltati sunt fluctus eius.
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
Ascendunt usque ad cælos, et descendunt usque ad abyssos: anima eorum in malis tabescebat.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
Turbati sunt, et moti sunt sicut ebrius: et omnis sapientia eorum devorata est.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur, et de necessitatibus eorum eduxit eos.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Et statuit procellam eius in auram: et siluerunt fluctus eius.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
Et lætati sunt quia siluerunt: et deduxit eos in portum voluntatis eorum.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Confiteantur Domino misericordiæ eius: et mirabilia eius filiis hominum.
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Et exaltent eum in Ecclesia plebis: et in cathedra seniorum laudent eum.
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Posuit flumina in desertum: et exitus aquarum in sitim.
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
Terram fructiferam in salsuginem, a malitia inhabitantium in ea.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Posuit desertum in stagna aquarum: et terram sine aqua in exitus aquarum.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
Et collocavit illic esurientes: et constituerunt civitatem habitationis.
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
Et seminaverunt agros, et plantaverunt vineas: et fecerunt fructum nativitatis.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Et benedixit eis, et multiplicati sunt nimis: et iumenta eorum non minoravit.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Et pauci facti sunt: et vexati sunt a tribulatione malorum, et dolore.
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
Effusa est contemptio super principes: et errare fecit eos in invio, et non in via.
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
Et adiuvit pauperem de inopia: et posuit sicut oves familias.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Videbunt recti, et lætabuntur: et omnis iniquitas oppilabit os suum.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Quis sapiens et custodiet hæc? et intelliget misericordias Domini?

< Zaburi 107 >