< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Praise ye Jah, give thanks to Jehovah, For good, for to the age, [is] His kindness.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Who doth utter the mighty acts of Jehovah? Soundeth all His praise?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
O the happiness of those keeping judgment, Doing righteousness at all times.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Remember me, O Jehovah, With the favour of Thy people, Look after me in Thy salvation.
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
To look on the good of Thy chosen ones, To rejoice in the joy of Thy nation, To boast myself with Thine inheritance.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
We have sinned with our fathers, We have done perversely, we have done wickedly.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Our fathers in Egypt, Have not considered wisely Thy wonders, They have not remembered The abundance of Thy kind acts, And provoke by the sea, at the sea of Suph.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
And He saveth them for His name's sake, To make known His might,
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
And rebuketh the sea of Suph, and it is dried up, And causeth them to go Through depths as a wilderness.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
And He saveth them from the hand Of him who is hating, And redeemeth them from the hand of the enemy.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
And waters cover their adversaries, One of them hath not been left.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
And they believe in His words, they sing His praise,
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
They have hasted — forgotten His works, They have not waited for His counsel.
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
And they lust greatly in a wilderness, And try God in a desert.
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
And He giveth to them their request, And sendeth leanness into their soul.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
And they are envious of Moses in the camp, Of Aaron, Jehovah's holy one.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
Earth openeth, and swalloweth up Dathan, And covereth over the company of Abiram.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
And fire burneth among their company, A flame setteth on fire the wicked.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
They make a calf in Horeb, And bow themselves to a molten image,
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
And change their Honour Into the form of an ox eating herbs.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
They have forgotten God their saviour, The doer of great things in Egypt,
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
Of wonderful things in the land of Ham, Of fearful things by the sea of Suph.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
And He saith to destroy them, Unless Moses, His chosen one, Had stood in the breach before Him, To turn back His wrath from destroying.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
And they kick against the desirable land, They have not given credence to His word.
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
And they murmur in their tents, They have not hearkened to the voice of Jehovah.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
And He lifteth up His hand to them, To cause them to fall in a wilderness,
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
And to cause their seed to fall among nations, And to scatter them through lands.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
And they are coupled to Baal-Peor, And eat the sacrifices of the dead,
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
And they provoke to anger by their actions, And a plague breaketh forth upon them,
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
And Phinehas standeth, and executeth judgment, And the plague is restrained,
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
And it is reckoned to him to righteousness, To all generations — unto the age.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
And they cause wrath by the waters of Meribah, And it is evil to Moses for their sakes,
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
For they have provoked his spirit, And he speaketh wrongfully with his lips.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
They have not destroyed the peoples, As Jehovah had said to them,
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
And mix themselves among nations, and learn their works,
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
And serve their idols, And they are to them for a snare.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
And they sacrifice their sons And their daughters to destroyers,
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
And they shed innocent blood — Blood of their sons and of their daughters, Whom they have sacrificed to idols of Canaan, And the land is profaned with blood.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
And they are defiled with their works, And commit whoredom in their habitual doings.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
And the anger of Jehovah Is kindled against His people, And He doth abominate His inheritance.
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
And giveth them into the hand of nations, And those hating them rule over them,
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
And their enemies oppress them, And they are humbled under their hand.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Many times He doth deliver them, And they rebel in their counsel, And they are brought low in their iniquity.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
And He looketh on their distress When He heareth their cry,
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
And remembereth for them His covenant, And is comforted, According to the abundance of His kindness.
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
And He appointeth them for mercies Before all their captors.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Save us, O Jehovah our God, and gather us from the nations, To give thanks to Thy holy name, To glory in Thy praise.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Blessed [is] Jehovah, God of Israel, From the age even unto the age. And all the people said, 'Amen, praise Jah!'

< Zaburi 106 >