< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
A Psalm of David. Kindness and judgment I sing, To Thee, O Jehovah, I sing praise.
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
I act wisely in a perfect way, When dost Thou come in unto me? I walk habitually in the integrity of my heart, In the midst of my house.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I set not before mine eyes a worthless thing, The work of those turning aside I have hated, It adhereth not to me.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
A perverse heart turneth aside from me, Wickedness I know not.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
Whoso slandereth in secret his neighbour, Him I cut off, The high of eyes and proud of heart, him I endure not.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
Mine eyes are on the faithful of the land, To dwell with me, Whoso is walking in a perfect way, he serveth me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
He dwelleth not in my house who is working deceit, Whoso is speaking lies Is not established before mine eyes.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
At morning I cut off all the wicked of the land, To cut off from the city of Jehovah All the workers of iniquity!

< Zaburi 101 >