< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
A psalm of David. I will sing of covenant faithfulness and justice; to you, Yahweh, I will sing praises.
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
I will walk in the way of integrity. Oh, when will you come to me? I will walk with integrity within my house.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I will not put wrongdoing before my eyes; I hate worthless evil; it will not cling to me.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
Perverse people will leave me; I am not loyal to evil.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
I will destroy whoever secretly slanders his neighbor. I will not tolerate anyone who has a proud demeanor and an arrogant attitude.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
I will look to the faithful of the land to sit at my side. Those who walk in the way of integrity may serve me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
Deceitful people will not remain within my house; liars will not be welcome before my eyes.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
Morning by morning I will destroy all the wicked from the land; I will remove all evildoers from the city of Yahweh.

< Zaburi 101 >