< Zaburi 101 >

1 Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
A Psalm of David. I will sing of mercy and justice; unto Thee, O LORD, will I sing praises.
2 Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
I will give heed unto the way of integrity; Oh when wilt Thou come unto me? I will walk within my house in the integrity of my heart.
3 Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
I will set no base thing before mine eyes; I hate the doing of things crooked; it shall not cleave unto me.
4 Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
A perverse heart shall depart from me; I will know no evil thing.
5 Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
Whoso slandereth his neighbour in secret, him will I destroy; whoso is haughty of eye and proud of heart, him will I not suffer.
6 Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
Mine eyes are upon the faithful of the land, that they may dwell with me; he that walketh in a way of integrity, he shall minister unto me.
7 Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
He that worketh deceit shall not dwell within my house; he that speaketh falsehood shall not be established before mine eyes.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.
Morning by morning will I destroy all the wicked of the land; to cut off all the workers of iniquity from the city of the LORD.

< Zaburi 101 >