< Zaburi 10 >

1 Kwa nini, Yahweh, unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati wa shida?
Why do you stand far off, Jehovah? Why do you hide yourself in times of trouble?
2 Kwa sababu ya majivuno yao, watu waovu waawakimbiza wanyonge; Basi tafadhari uwafanye waovu kunaswa kwa mipango yao wenyewe walioipanga.
In arrogance, the wicked hunt down the weak. They are caught in the schemes that they devise.
3 Kwa kuwa mtu mwovu hujivuna kwa tamaa yake ya ndani; yeye hufurahisha tamaa na kumtusi Yahweh.
For the wicked boasts of his heart's cravings, and he blesses the greedy, scorning Jehovah.
4 Mtu mwovu ameinua uso wake; naye hamtafuti Mungu. Yeye hamfikilii Mungu kamwe kwa kuwa hamjali kabisa Mungu.
The wicked in his proud countenance does not seek. All his thoughts are "There is no God."
5 Yeye yuko salama wakati wote, amri zako za haki ziko juu sana kwake; naye huwadharau adui zake wote.
His ways are firm at all times. Your judgments are turned aside. As for all his adversaries, he sneers at them.
6 Yeye husema moyoni mwake, “Siwezi kamwe kushindwa; katika kizazi chote sitakutana na shida.”
He says in his heart, "I shall not be shaken. From generation to generation I shall not experience calamity."
7 Mdomoni mwake kumejaa kulaani na udanganyifu, maneno yenye sumu; ulimi wake unajeruhi na kuharibu.
His mouth is full of cursing and bitterness and oppression. Under his tongue is mischief and iniquity.
8 Yeye husubilia kwenye shambulio karibu na kijiji; mahali pa siri huwauwa watu wasio na hatia; macho yake huwatazama wasionahatia.
He lies in wait near the villages. From ambushes, he murders the innocent. His eyes are secretly set against the helpless.
9 Hujibanza mahari pa siri kama simba katika kichaka; yeye hulala akisubiri kumkamata mnyonge. Humkamata pale anapokwisha mweka mtegoni mwake.
He lurks in secret as a lion in his ambush. He lies in wait to catch the helpless. He catches the helpless, when he draws him in his net.
10 Wanyonge wake hugandamizwa chini na kupigwa; wao huangukia katika mtego imara.
The helpless are crushed. They collapse. They fall under his strength.
11 Yeye husema katika moyo wake, “Mungu amesahau; huficha uso wake; hawezi kujishughulisha kutazama.”
He says in his heart, "God has forgotten. He hides his face. He will never see it."
12 Inuka, Yahweh! Inua mkono wako, Mungu! Usiwasahau wanyonge.
Arise, Jehovah. God, lift up your hand. Do not forget the helpless.
13 Kwa nini mtu mwovu anamkataa Mungu na kusema moyoni mwake, “Hautanipata katika hatia?”
Why does the wicked person condemn God, and say in his heart, "You will not seek (an accounting)."
14 Umeona, maana mara zote unaangalia mtu aletaye madhara na jeuri. Mtu asiye na msaada hukuachia nafsi yake; maana wewe huwaokoa yatima.
But you do see trouble and grief. You consider it to take it into your hand. You help the victim and the fatherless.
15 vunja mkono wa mwovu lo na mtu mwovu. Umuajibishe kwa matendo yake maovu, ambayo kwayo alifikiri hautayagundua.
Break the arm of the wicked. As for the evil man, seek out his wickedness until you find none.
16 Yahweh ni mfalme milele daima; mataifa yanaondolewa katika aridhi yake.
Jehovah is King forever and ever. The nations have perished from his land.
17 Yahweh, umesikia uhitaji wa wanyonge; nawe umeitia nguvu mioyo yao, wewe unasikia maombi;
Jehovah, you have heard the desire of the humble. You will prepare their heart. You will cause your ear to hear,
18 Unawatetea yatima na wanyonge ili kusudi pasiwepo na mtu katika dunia hii atakaye leta hofu tena.
to judge the fatherless and the oppressed, that man who is of the earth may terrify no more.

< Zaburi 10 >