< Mithali 7 >

1 Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
O son my keep words my and commandments my you will treasure with you.
2 Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
Keep commandments my and live and instruction my like [the] pupil of eyes your.
3 Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
Bind them on fingers your write them on [the] tablet of heart your.
4 Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
Say to wisdom [are] sister my you and a relative to discernment you will call.
5 ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
To keep you from a woman strange from a foreign [woman] [who] words her she makes smooth.
6 Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
For at [the] window of house my through lattice my I looked down.
7 Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
And I saw among the naive people I observed among the sons a youth lacking of heart.
8 Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
[who] was passing by In the street beside corner her and [the] direction of house her he strode.
9 Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
At twilight in [the] evening of [the] day in [the] middle of [the] night and darkness.
10 Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
And there! a woman to meet him [the] garment of a prostitute and guarded of heart.
11 Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
[is] boisterous She and rebellious in house her not they stay feet her.
12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
A time - in the street a time in the open places and beside every corner she lies in wait.
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
And she takes hold on him and she kisses him she has made firm face her and she said to him.
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
Sacrifices of peace offerings [are] on me this day I have paid vows my.
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
There-fore I have come out to meet you to seek face your and I have found you.
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
Coverings I have spread couch my colored fabrics linen of Egypt.
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
I have sprinkled bed my myrrh aloes and cinnamon.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
Come! let us take our fill of love until the morning let us delight ourselves with love.
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
For not the husband [is] in house his he has gone on a journey from a distance.
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
[the] bag of Money he has taken in hand his to [the] day of the full moon he will come house his.
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
She turns him with [the] greatness of persuasiveness her with [the] seductiveness of lips her she impels him.
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
[he is] walking Behind her suddenly like an ox [which] to [the] slaughter it goes and like an anklet to [the] chastening of a fool.
23 mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
Until it will pierce an arrow liver his as hurries a bird into a trap and not he knows that [is] for life his it.
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
And therefore O children listen to me and be attentive to [the] words of mouth my.
25 Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
May not it turn aside to ways her heart your may not it go astray in pathways her.
26 Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
For many slain [ones] she has made fall and [are] numerous all killed [men] her.
27 Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
[is] [the] ways of Sheol house her [which] go down to [the] chambers of death. (Sheol h7585)

< Mithali 7 >