< Mithali 31 >

1 Maneno ya mfalme Lemueli - mausia aliyofundishwa na mama yake.
Palabras del rey Lemuel, La profecía que le enseñó su madre:
2 Mwanangu nini? Na ni nini mwana wa tumbo langu? Na ni nini mwana wa nadhiri zangu?
¿Qué te diré, hijo mío? ¡Oh, hijo de mi vientre! ¿Qué te diré, hijo de mis votos?
3 Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
No des tu fuerza a las mujeres, Ni tus caminos al que destruye a los reyes.
4 Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
No es de reyes, oh Lemuel, Ni es de los reyes beber vino, Ni de los gobernantes el licor.
5 Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
No sea que al beber, olviden lo que se decretó, Y perviertan el derecho de todos los afligidos.
6 Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
Den el licor fuerte al desfallecido, Y el vino a los de ánimo amargado,
7 Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
Para que beban y olviden su necesidad, Y ya no se acuerden de su miseria.
8 Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
Abre tu boca a favor del mudo, Defiende la causa de todos los abandonados.
9 Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
Abre tu boca, juzga con justicia Y defiende al pobre y al necesitado.
10 Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
Mujer virtuosa, ¿quién la hallará? Porque su estima sobrepasa largamente a la de las piedras preciosas.
11 Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
El corazón de su esposo está confiado en ella, Y no carecerá de ganancias.
12 Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
Ella le dará bien y no mal Todos los días de su vida.
13 Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
Busca la lana y el lino, Y diligentemente trabaja con sus manos.
14 Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
Es como la nave del mercader, Que trae su pan desde lejos.
15 Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
Se levanta cuando aún es noche, Da alimento a su familia, Y la porción asignada a sus criadas.
16 Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
Evalúa un campo y lo compra, Y del fruto de sus manos planta una viña.
17 Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
Ciñe con firmeza su cintura, Y esfuerza sus brazos.
18 Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
Ve que sus negocios van bien. Su lámpara no se apaga de noche.
19 Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
Aplica sus manos a la rueca, Y sus dedos manejan el huso.
20 Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
Extiende su mano al pobre, Sí, alarga sus manos al necesitado.
21 Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
No tiene temor por su familia a causa de la nieve, Porque toda su familia lleva ropas dobles de color escarlata.
22 Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
Teje tapices para sí. De lino fino y púrpura es su vestido.
23 Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
Su esposo es conocido en la puerta Cuando se sienta con los ancianos de la tierra.
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
[Ella] hace ropa de lino y la vende, Y provee cinturones al mercader.
25 Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
Está vestida de fuerza y dignidad, Y sonríe ante el mañana.
26 Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
Abre su boca con sabiduría, Y la ley de la clemencia está en su lengua.
27 Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
Vigila la marcha de su casa, Y no come su pan de ociosidad.
28 Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
Sus hijos crecen, y la consideran inmensamente feliz, Su esposo también la alaba y dice:
29 “Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
Muchas mujeres hicieron el bien, Pero tú las superaste a todas.
30 Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
Engañosa es la gracia y vana la hermosura, La mujer que teme a Yavé será alabada.
31 Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.
¡Denle del fruto de sus manos, Y que sus mismas obras la alaben en la puerta!

< Mithali 31 >