< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usizisahau amri zangu na uyatunze mafundisho yangu katika moyo wako, 2 maana ziatakuongezea siku zako na miaka ya maisha yako na amani. 3 Usiache utiifu wa agano na uaminifu viondoke kwako, vifunge katika shingo yako, viandike katika vibao vya moyo wako. 4 Ndipo utapata kibali na heshima mbele Mungu na wanadamu. 5 Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote na wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe, 6 katika njia zako zote mkiri Yeye na yeye atayanyosha mapito yako. 7 Usiwe mwenye busara machoni pako mwenyewe; mche Yehova na jiepushe na uovu. 8 Itakuponya mwili wako na kukuburudisha mwili wako. 9 Mheshimu Yehova kwa utajiri wako na kwa malimbuko ya mazao kwa kila unachozalisha, 10 na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya. 11 Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake, 12 maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye. 13 Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu. 14 Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu. 15 Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima. 16 Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima. 17 Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani. 18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha. 19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu. 20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake. 21 Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama. 22 Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako. 23 Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa; 24 ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu. 25 Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea, 26 kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego. 27 Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako. 28 Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo. 29 Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini. 30 Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru. 31 Usimhusudu mtu jeuri au kuchagua njia zake zozote. 32 Maana mtu mjanja ni chukizo kwa Yehova, bali humleta mtu mwaminifu kwenye tumaini lake. 33 Laana ya Yehova ipo katika nyumba ya watu waovu, bali huibariki maskani ya watu wenye haki. 34 Yeye huwadhihaki wenye dhihaka, bali huwapa hisani watu wanyenyekevu. 35 Watu wenye busara huirithi heshima, bali wapumbavu huinuliwa kwa fedheha yao wenyewe.

< Mithali 3 >