< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
Huye el impío sin que nadie lo persiga, Pero como león está confiado el justo.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
Por la rebelión de la tierra sus jefes son muchos, Pero por el hombre entendido y sabio permanece estable.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
El hombre pobre que explota a los indigentes Es como lluvia torrencial que no deja pan.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Los que abandonan la Ley alaban al impío. Los que la guardan contienden con ellos.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Los perversos no entienden la justicia, Pero el que busca a Yavé lo entiende todo.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Mejor es el pobre que anda en su integridad, Que rico de caminos torcidos.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
El que observa la Ley es hijo inteligente, El que se reúne con glotones avergüenza a su padre.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
El que aumenta su fortuna con interés y usura Acumula para el que se compadece de los pobres.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Al que aparta su oído para no oír la Ley, Aun su oración es una repugnancia.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
El que extravía al recto por el mal camino Caerá en su propia fosa, Pero los íntegros heredarán el bien.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
El hombre rico es sabio en su propia opinión, Pero el entendido pobre lo escudriña.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
Cuando triunfa el justo hay gran esplendor, Cuando se yerguen los impíos, los hombres se esconden.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
El que encubre sus pecados no prosperará, Pero el que los confiesa y se aparta alcanzará misericordia.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
¡Inmensamente feliz es el hombre que teme siempre! Pero el que endurece su corazón caerá en la desgracia.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
León rugiente y oso hambriento, Es el gobernante impío sobre un pueblo pobre.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
El gobernante falto de entendimiento aumenta la extorsión, Pero el que aborrece la avaricia alargará sus días.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
El hombre culpable de homicidio hacia la fosa huye. ¡Nadie lo detenga!
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
El que anda en integridad será librado, Pero el que oscila entre dos caminos caerá de repente.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
El que labra su tierra se saciará de pan, Pero el que persigue vanidades se hartará de pobreza.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
El hombre leal tendrá muchas bendiciones, Pero el que se apresura a enriquecerse no quedará impune.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
Hacer acepción de personas no es bueno, Pero, ¡hasta por un bocado de pan puede transgredir un hombre!
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
El hombre de mirada desleal se afana por enriquecer, Y no sabe que lo alcanzará la miseria.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
El que reprende al hombre hallará mayor gracia Que el de boca lisonjera.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
El que roba a padre o madre y dice que no es pecado, Es compañero del destructor.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
El arrogante suscita contiendas, Pero el que confía en Yavé prosperará.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
El que confía en su propio corazón es un necio, Pero el que anda en sabiduría será librado.
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
El que da al pobre no tendrá necesidad, Pero el que aparta de él sus ojos tendrá muchas maldiciones.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Cuando se levantan los perversos, los hombres se esconden, Pero cuando perecen, aumentan los justos.

< Mithali 28 >