< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
Quomodo nix in æstate, et pluviæ in messe: sic indecens est stulto gloria.
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
Sicut avis ad alia transvolans, et passer quo libet vadens: sic maledictum frustra prolatum in quempiam superveniet.
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
Flagellum equo, et camus asino, et virga in dorso imprudentium.
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
Ne respondeas stulto iuxta stultitiam suam, ne efficiaris ei similis.
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
Responde stulto iuxta stultitiam suam, ne sibi sapiens esse videatur.
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
Claudus pedibus, et iniquitatem bibens, qui mittit verba per nuncium stultum.
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Quomodo pulchras frustra habet claudus tibias: sic indecens est in ore stultorum parabola.
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
Sicut qui mittit lapidem in acervum Mercurii: ita qui tribuit insipienti honorem.
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Quomodo si spina nascatur in manu temulenti: sic parabola in ore stultorum.
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
Iudicium determinat causas: et qui imponit stulto silentium, iras mitigat.
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
Sicut canis, qui revertitur ad vomitum suum, sic imprudens, qui iterat stultitiam suam.
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
Vidisti hominem sapientem sibi videri? magis illo spem habebit insipiens.
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
Dicit piger: Leo est in via, et leæna in itineribus:
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
sicut ostium vertitur in cardine suo, ita piger in lectulo suo.
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
Abscondit piger manum sub ascella sua, et laborat si ad os suum eam converterit.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
Sapientior sibi piger videtur septem viris loquentibus sententias.
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
Sicut qui apprehendit auribus canem, sic qui transit impatiens, et commiscetur rixæ alterius.
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
Sicut noxius est qui mittit sagittas, et lanceas in mortem:
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
ita vir, fraudulenter nocet amico suo: et cum fuerit deprehensus, dicit: Ludens feci.
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
Cum defecerint ligna, extinguetur ignis: et susurrone subtracto, iurgia conquiescent.
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
Sicut carbones ad prunas, et ligna ad ignem, sic homo iracundus suscitat rixas.
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
Verba susurronis quasi simplicia, et ipsa perveniunt ad intima ventris.
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
Quomodo si argento sordido ornare velis vas fictile, sic labia tumentia cum pessimo corde sociata.
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
Labiis suis intelligitur inimicus, cum in corde tractaverit dolos.
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
Quando submiserit vocem suam, ne credideris ei: quoniam septem nequitiæ sunt in corde illius.
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
Qui operit odium fraudulenter, revelabitur malitia eius in consilio.
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
Qui fodit foveam, incidet in eam: et qui volvit lapidem, revertetur ad eum.
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
Lingua fallax non amat veritatem: et os lubricum operatur ruinas.

< Mithali 26 >