< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
As snow in summer, and as rain in harvest, so honour is not seemly for a fool.
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
As the sparrow in her wandering, as the swallow in her flying, so the curse that is causeless lighteth not.
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
A whip for the horse, a bridle for the ass, and a rod for the back of fools.
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
Answer not a fool according to his folly, lest thou also be like unto him.
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
Answer a fool according to his folly, lest he be wise in his own conceit.
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
He that sendeth a message by the hand of a fool cutteth off [his own] feet, [and] drinketh in damage.
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
The legs of the lame hang loose: so is a parable in the mouth of fools.
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
As a bag of gems in a heap of stones, so is he that giveth honour to a fool.
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
[As] a thorn that goeth up into the hand of a drunkard, so is a parable in the month of fools.
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
[As] an archer that woundeth all, so is he that hireth the fool and he that hireth them that pass by.
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
As a dog that returneth to his vomit, [so is] a fool that repeateth his folly.
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
Seest thou a man wise in his own conceit? there is more hope of a fool than of him.
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
The sluggard saith, There is a lion in the way; a lion is in the streets.
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
[As] the door turneth upon its hinges, so doth the sluggard upon his bed.
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
The sluggard burieth his hand in the dish; it wearieth him to bring it again to his mouth.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
The sluggard is wiser in his own conceit than seven men that can render a reason.
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
He that passeth by, [and] vexeth himself with strife belonging not to him, is [like] one that taketh a dog by the ears.
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
As a madman who casteth firebrands, arrows, and death;
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
So is the man that deceiveth his neighbour, and saith, Am not I in sport?
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
For lack of wood the fire goeth out: and where there is no whisperer, contention ceaseth.
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
[As] coals are to hot embers, and wood to fire; so is a contentious man to inflame strife.
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
The words of a whisperer are as dainty morsels, and they go down into the innermost parts of the belly.
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
Fervent lips and a wicked heart are [like] an earthen vessel overlaid with silver dross.
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
He that hateth dissembleth with his lips, but he layeth up deceit within him:
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
When he speaketh fair, believe him not; for there are seven abominations in his heart:
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
Though [his] hatred cover itself with guile, his wickedness shall be openly shewed before the congregation.
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
Whoso diggeth a pit shall fall therein: and he that rolleth a stone, it shall return upon him.
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
A lying tongue hateth those whom it hath wounded; and a flattering mouth worketh ruin.

< Mithali 26 >