< Mithali 25 >

1 Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
اینها نیز از امثال سلیمان است که مردان حزقیا، پادشاه یهودا آنها را نقل نمودند.۱
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
مخفی داشتن امر جلال خدا است، و تفحص نمودن امر جلال پادشاهان است.۲
3 Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
آسمان را در بلندیش و زمین را در عمقش، ودل پادشاهان را تفتیش نتوان نمود.۳
4 Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
درد را از نقره دور کن، تا ظرفی برای زرگربیرون آید.۴
5 Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
شریران را از حضور پادشاه دور کن، تاکرسی او در عدالت پایدار بماند.۵
6 Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
در حضور پادشاه خویشتن را برمیفراز، و درجای بزرگان مایست،۶
7 Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
زیرا بهتر است تو را گفته شود که اینجا بالابیا، از آنکه به حضور سروری که چشمانت او رادیده است تو را پایین برند.۷
8 Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
برای نزاع به تعجیل بیرون مرو، مبادا درآخرش چون همسایه ات تو را خجل سازد، ندانی که چه باید کرد.۸
9 Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
دعوی خود را با همسایه ات بکن، اما رازدیگری را فاش مساز،۹
10 au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
مبادا هر‌که بشنود تو را ملامت کند، وبدنامی تو رفع نشود.۱۰
11 Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
سخنی که در محلش گفته شود، مثل سیبهای طلا در مرصعکاری نقره است.۱۱
12 Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
مودب حکیم برای گوش شنوا، مثل حلقه طلا و زیور زر خالص است.۱۲
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
رسول امین برای فرستندگان خود، چون خنکی یخ در موسم حصاد می‌باشد، زیرا که جان آقایان خود را تازه می‌کند.۱۳
14 Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
کسی‌که از بخششهای فریبنده خود فخرمی کند، مثل ابرها و باد بی‌باران است.۱۴
15 Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
با تحمل داور را به رای خود توان آورد، وزبان ملایم، استخوان را می‌شکند.۱۵
16 Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
اگر عسل یافتی بقدر کفایت بخور، مبادا ازآن پر شده، قی کنی.۱۶
17 Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
پای خود را از زیاد رفتن به خانه همسایه ات باز دار، مبادا از تو سیر شده، از تونفرت نماید.۱۷
18 Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
کسی‌که درباره همسایه خود شهادت دروغ دهد، مثل تبرزین و شمشیر و تیر تیز است.۱۸
19 Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
اعتماد بر خیانتکار در روز تنگی، مثل دندان کرم زده و پای مرتعش می‌باشد.۱۹
20 Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
سراییدن سرودها برای دلتنگ، مثل کندن جامه در وقت سرما و ریختن سرکه بر شوره است.۲۰
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
اگر دشمن تو گرسنه باشد او را نان بخوران، و اگر تشنه باشد او را آب بنوشان،۲۱
22 maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
زیرا اخگرها بر سرش خواهی انباشت، وخداوند تو را پاداش خواهد داد.۲۲
23 Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
چنانکه باد شمال باران می‌آورد، همچنان زبان غیبتگو چهره را خشمناک می‌سازد.۲۳
24 Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
ساکن بودن در گوشه پشت بام بهتر است ازبودن با زن جنگجو در خانه مشترک.۲۴
25 Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
خبر خوش از ولایت دور، مثل آب سردبرای جان تشنه است.۲۵
26 Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
مرد عادل که پیش شریر خم شود، مثل چشمه گل آلود و منبع فاسد است.۲۶
27 Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
زیاد عسل خوردن خوب نیست، همچنان طلبیدن جلال خود جلال نیست.۲۷
28 Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.
کسی‌که بر روح خود تسلط ندارد، مثل شهر منهدم و بی‌حصار است.۲۸

< Mithali 25 >