< Mithali 24 >

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
No tengas envidia de los hombres malvados; ni ansia de estar con ellos;
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
porque su corazón maquina rapiñas, y sus labios hablan para dañar.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
Con la sabiduría se edifica una casa, y con la prudencia se afirma.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
Con la inteligencia se hinchen sus cámaras de todo lo más precioso y deseable.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
El hombre sabio está lleno de fuerza; el que tiene sabiduría aumenta su poder.
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
Pues con prudentes medidas puedes ganar la guerra, y donde hay muchos consejeros allí está la victoria.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
Cosa demasiado alta es para el necio la sabiduría; no abrirá él en el foro su boca.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
Quien medita cómo hacer daño será llamado intrigante.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
El afán del insensato consiste en pecar, y abominable para los hombres es el maldiciente.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
Si desfalleces en el día de la prueba, tu fortaleza es poca cosa.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
Libra a los que son llevados a la muerte; a los que andan vacilando al degolladero, sálvalos.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Si dijeres: “¿Cómo saberlo?” ¿Acaso no lo ve Aquel que pesa los corazones? Bien lo sabe Aquel que vela sobre tu vida; Él retribuirá a cada cual según sus obras.
13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
Come, hijo mío, miel, porque es buena, y el panal, que es dulce para tu paladar.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
Tal será para tu alma la sabiduría; si la hallares, el porvenir será tuyo, y tu esperanza no será frustrada.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
No pongas, malvado, asechanzas a la morada del justo, ni devastes el lugar de su reposo.
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
El justo se levanta, aunque caiga siete veces, los impíos, empero, se pierden en el mal.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
No te goces en la caída de tu enemigo; si sucumbe no se alegre tu corazón,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
no sea que al verlo Yahvé se ofenda y aparte de sobre él su enojo.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
No te irrites a causa de los impíos, ni envidies a los malhechores.
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
Porque no hay porvenir para el malo; la lámpara de los impíos se apagará.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
Hijo mío, teme a Yahvé y al rey, y no te asocies con los revoltosos;
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
porque de repente vendrá sobre ellos su ruina, y la desventura de ambos, ¿quién la conoce?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
También estas son sentencias de los sabios: Es cosa mala hacer acepción de personas en el juicio.
24 Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
Quien dice al delincuente: “Tú tienes razón”, será maldito del pueblo y detestado de la gente.
25 Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
Y aquellos que lo condenan, serán alabados, y sobre ellos vienen ricas bendiciones.
26 Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
Los labios besa quien responde palabras rectas.
27 Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
Haz con esmero tu trabajo de afuera, aplicándolo a tu campo, y luego podrás edificar tu casa.
28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
No seas de ligero testigo contra tu prójimo; ¿quieres acaso engañarlo con tus labios?
29 Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
No digas: “Como él me trató, así haré con él, le daré el pago según sus obras.”
30 Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
Pasé junto al campo del perezoso, y junto a la viña del insensato;
31 Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
y he aquí que espinas brotaban por todas partes, ortigas cubrían su superficie y la cerca de piedra estaba destruida.
32 Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
Lo vi y me puse a reflexionar; lo miré y aprendí esta lección:
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
Un poco dormir, un poco dormitar, cruzar un poco las manos para descansar,
34 na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.
y sobrevendrá cual salteador la miseria, y como hombre armado, la necesidad.

< Mithali 24 >