< Mithali 22 >

1 Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
[is to be] chosen A name more than wealth great more than silver and more than gold favor good.
2 Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
[the] rich And [the] poor they meet together [is the] maker of all of them Yahweh.
3 Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
A sensible [person] - he sees trouble (and he hides himself *Qk) and naive people they pass on and they are punished.
4 Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
[the] consequence of Humility [the] fear of Yahweh [is] wealth and honor and life.
5 Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
Thorns snares [are] in [the] path of a perverse [person] [one who] guards self his he will be far from them.
6 Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
Train the youth on [the] mouth of way his also if he will be old not he will turn aside from it.
7 Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
A rich [person] over poor [people] he rules and [is] a servant a borrower of a person a lender.
8 Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
[one who] sows Unrighteousness (he will reap *Qk) trouble and [the] rod of fury his it will end.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
A [person] good of eye he he will be blessed for he gives some of food his to poor [person].
10 Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
Drive out a mocker so may go out strife so may cease dispute and shame.
11 Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
[one who] loves (Pure of *Qk) heart [the] grace of lips his [is] friend his a king.
12 Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
[the] eyes of Yahweh they preserve knowledge and he has subverted [the] words of [one who] acts treacherously.
13 Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
He says a sluggard a lion [is] in the street in [the] midst of [the] open places I will be killed.
14 Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
[is] a pit Deep [the] mouth of strange [women] [one who] is cursed of Yahweh (he will fall *Qk) there.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
Foolishness [is] bound in [the] heart of a youth a rod of discipline it will put far away it from him.
16 Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
[one who] oppresses [the] poor To increase for himself [one who] gives to a rich [person] only to poverty.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
Incline ear your and hear [the] words of wise [people] and heart your you will set to knowledge my.
18 maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
For [will be] pleasant that you will keep them in belly your they will be prepared together on lips your.
19 Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
To be in Yahweh trust your I teach you this day even you.
20 Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
¿ Not have I written for you (officers *QK) counsels and knowledge.
21 kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
To make known to you [the] truth of words of faithfulness to bring back words faithfulness to [those who] sent you.
22 Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
May not you rob a poor [person] for [is] poor he and may not you crush a poor [person] at the gate.
23 maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
For Yahweh he will conduct case their and he will rob [those who] rob them life.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
May not you associate with a master of anger and with a person of rage not you must go.
25 au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
Lest you should learn (ways his *QK) and you will take a snare for self your.
26 Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
May not you be among [those who] strike a palm among [those who] stand surety for debts.
27 Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
If not [belongs] to you to pay why? will anyone take bed your from under you.
28 Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
May not you displace a boundary of antiquity which they made ancestors your.
29 Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
You see a person - skilled in work his before kings he will take his stand not he will take his stand before insignificant [people].

< Mithali 22 >