< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda. 2 Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo. 3 Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka. 4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi. 5 Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini. 6 Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha. 7 Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki. 8 Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki. 9 Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi. 10 Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake. 11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa. 12 Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu. 13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa. 14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu. 15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya. 16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu. 17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri. 18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu. 19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko. 20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu. 21 Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima. 22 Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini. 23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu. 24 Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai. 25 Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi. 26 Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii. 27 Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya. 28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote. 29 Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake. 30 Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova. 31 Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Mithali 21 >