< Mithali 18 >

1 Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
El que se desvía busca su propio deseo, Y se enfada contra todo consejo.
2 Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
El necio no se deleita en el entendimiento, Sino solo en exponer lo que piensa.
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
Cuando viene la impiedad viene también el desprecio, Y con la deshonra viene la afrenta.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
Las palabras de la boca de un hombre son aguas profundas, Torrente caudaloso es la fuente de la sabiduría.
5 Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
No es bueno mostrar preferencia por el perverso, Para desviar al justo en el juicio.
6 Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
Los labios del necio traen contienda, Y su boca clama por azotes.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
La boca del necio es su ruina, Y sus labios, trampa para su alma.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
Las palabras del chismoso son como delicados manjares Que penetran hasta el fondo de sus órganos internos.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
El negligente en su obra es hermano del disipador.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
Torre fuerte es el Nombre de Yavé. A ella corre el justo y está a salvo.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
Las riquezas del rico son su ciudad fortificada, Como un alto muro en su imaginación.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
Antes del quebrantamiento el corazón del hombre es altivo, Y antes de la honra está la humildad.
13 Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
Al que responde antes de escuchar, Le es insensatez y deshonra.
14 Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
El buen ánimo del hombre soporta su enfermedad, Pero el ánimo abatido, ¿quién lo soportará?
15 Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
El corazón del entendido adquiere conocimiento, Y conocimiento busca el oído de los sabios.
16 Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
El regalo de un hombre le abre camino Y lo conduce a la presencia de los grandes.
17 Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
El primero que se defiende parece ser justo, Hasta que llega su prójimo y lo investiga.
18 Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
Echar suerte pone fin a la disputa, Y decide entre los poderosos.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
El hermano ofendido es más tenaz que ciudad fuerte, Y los litigios, más que los cerrojos de una fortaleza.
20 Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
Con el fruto de la boca del hombre llenará su estómago. Con el producto de sus labios se saciará.
21 Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
La muerte y la vida están en poder de la boca. El que la ama comerá su fruto.
22 Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
El que halla esposa halla el bien, Y alcanza el favor de Yavé.
23 Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
El pobre se expresa con súplicas, El rico responde con durezas.
24 Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.
Hay amigos que causan ruina al hombre, Pero hay un amigo más fiel que un hermano.

< Mithali 18 >