< Mithali 18 >

1 Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
Occasiones quærit qui vult recedere ab amico: omni tempore erit exprobrabilis.
2 Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
Non recipit stultus verba prudentiæ: nisi ea dixeris quæ versantur in corde eius.
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
Impius, cum in profundum venerit peccatorum, contemnit: sed sequitur eum ignominia et opprobrium.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
Aqua profunda verba ex ore viri: et torrens redundans fons sapientiæ.
5 Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
Accipere personam impii non est bonum, ut declines a veritate iudicii.
6 Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
Labia stulti miscent se rixis: et os eius iurgia provocat.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
Os stulti contritio eius: et labia ipsius, ruina animæ eius.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
Verba bilinguis, quasi simplicia: et ipsa perveniunt usque ad interiora ventris. Pigrum deiicit timor: animæ autem effeminatorum esurient.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
Qui mollis et dissolutus est in opere suo, frater est sua opera dissipantis.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
Turris fortissima, nomen Domini: ad ipsum currit iustus, et exaltabitur.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
Substantia divitis urbs roboris eius, et quasi murus validus circumdans eum.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
Antequam conteratur, exaltatur cor hominis: et antequam glorificetur, humiliatur.
13 Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
Qui prius respondet quam audiat, stultum se esse demonstrat, et confusione dignum.
14 Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
Spiritus viri sustentat imbecillitatem suam: spiritum vero ad irascendum facilem quis poterit sustinere?
15 Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
Cor prudens possidebit scientiam: et auris sapientium quærit doctrinam.
16 Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
Donum hominis dilatat viam eius, et ante principes spatium ei facit.
17 Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
Iustus, prior est accusator sui: venit amicus eius, et investigabit eum.
18 Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
Contradictiones comprimit sors, et inter potentes quoque diiudicat.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
Frater, qui adiuvatur a fratre, quasi civitas firma: et iudicia quasi vectes urbium.
20 Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
De fructu oris viri replebitur venter eius: et genimina labiorum ipsius saturabunt eum.
21 Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
Mors, et vita in manu linguæ: qui diligunt eam, comedent fructus eius.
22 Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
Qui invenit mulierem bonam, invenit bonum: et hauriet iucunditatem a Domino. Qui expellit mulierem bonam, expellit bonum: qui autem tenet adulteram, stultus est et impius.
23 Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
Cum obsecrationibus loquetur pauper: et dives effabitur rigide.
24 Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.
Vir amabilis ad societatem, magis amicus erit, quam frater.

< Mithali 18 >