< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
The preparations of the heart are man's, but the answer of the tongue is from the LORD.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
All the ways of a man are clean in his own eyes; but the LORD weigheth the spirits.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Commit thy works unto the LORD, and thy thoughts shall be established.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
The LORD hath made every things for His own purpose, yea, even the wicked for the day of evil.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Every one that is proud in heart is an abomination to the LORD; my hand upon it! he shall not be unpunished.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
By mercy and truth iniquity is expiated; and by the fear of the LORD men depart from evil.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
When a man's ways please the LORD, He maketh even his enemies to be at peace with him.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Better is a little with righteousness than great revenues with injustice.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
A man's heart deviseth his way; but the LORD directeth his steps.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
A divine sentence is in the lips of the king; his mouth trespasseth not in judgment.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
A just balance and scales are the LORD'S; all the weights of the bag are His work.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
It is an abomination to kings to commit wickedness; for the throne is established by righteousness.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Righteous lips are the delight of kings; and they love him that speaketh right.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
The wrath of a king is as messengers of death; but a wise man will pacify it.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
In the light of the king's countenance is life; and his favour is as a cloud of the latter rain.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
How much better is it to get wisdom than gold! yea, to get understanding is rather to be chosen than silver.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
The highway of the upright is to depart from evil; he that keepeth his way preserveth his soul.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pride goeth before destruction, and a haughty spirit before a fall.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Better it is to be of a lowly spirit with the humble, than to divide the spoil with the proud.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
He that giveth heed unto the word shall find good; and whoso trusteth in the LORD, happy is he.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
The wise in heart is called a man of discernment; and the sweetness of the lips increaseth learning.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Understanding is a fountain of life unto him that hath it; but folly is the chastisement of fools.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
The heart of the wise teacheth his mouth, and addeth learning to his lips.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Pleasant words are as a honeycomb, sweet to the soul, and health to the bones.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
There is a way which seemeth right unto a man, but the end thereof are the ways of death.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
The hunger of the labouring man laboureth for him; for his mouth compelleth him.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
An ungodly man diggeth up evil, and in his lips there is as a burning fire.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
A froward man soweth strife; and a whisperer separateth familiar friends.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
A man of violence enticeth his neighbour, and leadeth him into a way that is not good.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
He that shutteth his eyes, it is to devise froward things; he that biteth his lips bringeth evil to pass.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
The hoary head is a crown of glory, it is found in the way of righteousness.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
He that is slow to anger is better than the mighty; and he that ruleth his spirit than he that taketh a city.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
The lot is cast into the lap; but the whole disposing thereof is of the LORD.

< Mithali 16 >