< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
هر زن حکیم خانه خود را بنا می‌کند، اما زن جاهل آن را با دست خود خراب می‌نماید.۱
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
کسی‌که به راستی خود سلوک می‌نماید ازخداوند می‌ترسد، اما کسی‌که در طریق خودکج رفتار است او را تحقیر می‌نماید.۲
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
در دهان احمق چوب تکبر است، اما لبهای حکیمان ایشان را محافظت خواهد نمود.۳
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
جایی که گاو نیست، آخور پاک است، اما ازقوت گاو، محصول زیاد می‌شود.۴
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
شاهد امین دروغ نمی گوید، اما شاهد دروغ به کذب تنطق می‌کند.۵
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
استهزاکننده حکمت را می‌طلبد و نمی یابد. اما به جهت مرد فهیم علم آسان است.۶
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
از حضور مرد احمق دور شو، زیرا لبهای معرفت را در او نخواهی یافت.۷
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
حکمت مرد زیرک این است که راه خود رادرک نماید، اما حماقت احمقان فریب است.۸
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
احمقان به گناه استهزا می‌کنند، اما در میان راستان رضامندی است.۹
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
دل شخص تلخی خویشتن را می‌داند، وغریب در خوشی آن مشارکت ندارد.۱۰
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
خانه شریران منهدم خواهد شد، اما خیمه راستان شکوفه خواهد آورد.۱۱
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
راهی هست که به نظر آدمی مستقیم می‌نماید، اما عاقبت آن، طرق موت است.۱۲
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
هم در لهو و لعب دل غمگین می‌باشد، وعاقبت این خوشی حزن است.۱۳
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
کسی‌که در دل مرتد است از راههای خودسیر می‌شود، و مرد صالح به خود سیر است.۱۴
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
مرد جاهل هر سخن را باور می‌کند، اما مردزیرک در رفتار خود تامل می‌نماید.۱۵
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
مرد حکیم می‌ترسد و از بدی اجتناب می‌نماید، اما احمق از غرور خود ایمن می‌باشد.۱۶
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
مرد کج خلق، احمقانه رفتار می‌نماید، و(مردم ) از صاحب سوظن نفرت دارند.۱۷
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
نصیب جاهلان حماقت است، اما معرفت، تاج زیرکان خواهد بود.۱۸
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
بدکاران در حضور نیکان خم می‌شوند، وشریران نزد دروازه های عادلان می‌ایستند.۱۹
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
همسایه فقیر نیز از او نفرت دارد، امادوستان شخص دولتمند بسیارند.۲۰
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
هر‌که همسایه خود را حقیر شمارد گناه می‌ورزد، اما خوشابحال کسی‌که بر فقیران ترحم نماید.۲۱
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
آیا صاحبان تدبیر فاسد گمراه نمی شوند، اما برای کسانی که تدبیر نیکو می‌نمایند، رحمت و راستی خواهد بود.۲۲
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
از هر مشقتی منفعت است، اما کلام لبها به فقر محض می‌انجامد.۲۳
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
تاج حکیمان دولت ایشان است، اماحماقت احمقان حماقت محض است.۲۴
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
شاهد امین جانها را نجات می‌بخشد، اما هرکه به دروغ تنطق می‌کند فریب محض است.۲۵
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
در ترس خداوند اعتماد قوی است، وفرزندان او را ملجا خواهد بود.۲۶
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
ترس خداوند چشمه حیات‌است، تا ازدامهای موت اجتناب نمایند.۲۷
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
جلال پادشاه از کثرت مخلوق است، وشکستگی سلطان از کمی مردم است.۲۸
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
کسی‌که دیرغضب باشد کثیرالفهم است، وکج خلق حماقت را به نصیب خود می‌برد.۲۹
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
دل آرام حیات بدن است، اما حسدپوسیدگی استخوانها است.۳۰
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
هر‌که بر فقیر ظلم کند آفریننده خود راحقیر می‌شمارد، و هر‌که بر مسکین ترحم کند اورا تمجید می‌نماید.۳۱
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
شریر از شرارت خود به زیر افکنده می‌شود، اما مرد عادل چون بمیرد اعتماد دارد.۳۲
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
حکمت در دل مرد فهیم ساکن می‌شود، امادر اندرون جاهلان آشکار می‌گردد.۳۳
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
عدالت قوم را رفیع می‌گرداند، اما گناه برای قوم، عار است.۳۴
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
رضامندی پادشاه بر خادم عاقل است، اماغضب او بر پست فطرتان.۳۵

< Mithali 14 >