< Mithali 13 >

1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
Mądry syn [przyjmuje] pouczenie ojca, a szyderca nie słucha strofowania.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
Człowiek będzie spożywać dobro z owocu swoich ust, a dusza przewrotnych [będzie spożywać] przemoc.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
Kto strzeże swych ust, strzeże swojej duszy; kto [szeroko] otwiera swe wargi, będzie zniszczony.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
Dusza leniwego pragnie, a nic nie ma, a dusza pracowitych zostanie obficie nasycona.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
Sprawiedliwy nienawidzi kłamliwego słowa, a niegodziwy staje się obrzydliwy i zhańbiony.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Sprawiedliwość strzeże tego, który postępuje uczciwie, a niegodziwość powala grzesznika.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
Znajduje się taki, który czyni siebie bogatym, a nie ma nic; inny czyni siebie ubogim, choć ma wiele bogactw.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
Okupem za życie człowieka jest jego bogactwo, a ubogi nie słucha strofowania.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
Radośnie błyszczy światło sprawiedliwych, a pochodnia niegodziwych zgaśnie.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
Spór powstaje tylko dzięki pysze, a mądrość jest przy tych, co przyjmują radę.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Łatwo zdobyte bogactwo zmniejsza się, a kto je gromadzi [swą] ręką, pomnaża je.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Przedłużająca się nadzieja sprawia ból sercu, a spełnione pragnienie [jest] drzewem życia.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
Kto gardzi słowem [Bożym], ten zginie, a kto się boi przykazania, dostanie nagrodę.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
Prawo mądrego jest źródłem życia, by uniknąć sideł śmierci.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Prawdziwy rozum daje łaskę, a droga przewrotnych jest ciężka.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Każdy roztropny postępuje rozważnie, a głupi ujawnia głupotę.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
Niegodziwy posłaniec popada w zło, a wierny wysłannik jest lekarstwem.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Ubóstwo i hańba [spadną na] tego, który odrzuca karność, a kto szanuje upomnienia, dozna czci.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
Spełnione pragnienie jest słodkie dla duszy, a odwrócenie się od zła budzi odrazę w głupcach.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
Kto przestaje z mądrymi, będzie mądry, a towarzysz głupców będzie zniszczony.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Nieszczęście ściga grzeszników, a sprawiedliwych [Bóg] nagrodzi dobrem.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
Dobry [człowiek] zostawia dziedzictwo dzieciom [swoich] dzieci, a majątek grzesznika jest zachowany dla sprawiedliwego.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Obfita żywność jest na roli ubogich, lecz i ta może niszczeć przez nieroztropność.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
Kto oszczędza swą rózgę, nienawidzi swego syna, a kto go kocha, karze w porę.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
Sprawiedliwy je i syci swoją duszę, a żołądek niegodziwych cierpi niedostatek.

< Mithali 13 >