< Mithali 13 >

1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
Filius sapiens, doctrina patris: qui autem illusor est, non audit cum arguitur.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
De fructu oris sui homo satiabitur bonis: anima autem prævaricatorum iniqua.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
Qui custodit os suum, custodit animam suam: qui autem inconsideratus est ad loquendum, sentiet mala.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
Vult et non vult piger: anima autem operantium impinguabitur.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
Verbum mendax iustus detestabitur: impius autem confundit, et confundetur.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Iustitia custodit innocentis viam: impietas autem peccatorem supplantat.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
Est quasi dives cum nihil habeat: et est quasi pauper, cum in multis divitiis sit.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
Redemptio animæ viri, divitiæ suæ: qui autem pauper est, increpationem non sustinet.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
Lux iustorum lætificat: lucerna autem impiorum extinguetur.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
Inter superbos semper iurgia sunt: qui autem agunt omnia cum consilio, reguntur sapientia.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Substantia festinata minuetur: quæ autem paulatim colligitur manu, multiplicabitur.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Spes, quæ differtur, affligit animam: lignum vitæ desiderium veniens.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
Qui detrahit alicui rei, ipse se in futurum obligat: qui autem timet præceptum, in pace versabitur. Animæ dolosæ errant in peccatis: iusti autem misericordes sunt, et miserantur.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
Lex sapientis fons vitæ, ut declinet a ruina mortis.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Doctrina bona dabit gratiam: in itinere contemptorum vorago.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Astutus omnia agit cum consilio: qui autem fatuus est, aperit stultitiam.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
Nuncius impii cadet in malum: legatus autem fidelis, sanitas.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Egestas, et ignominia ei, qui deserit disciplinam: qui autem acquiescit arguenti, glorificabitur.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
Desiderium si compleatur, delectat animam: detestantur stulti eos, qui fugiunt mala.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
Qui cum sapientibus graditur, sapiens erit: amicus stultorum similis efficietur.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Peccatores persequitur malum: et iustis retribuentur bona.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
Bonus reliquit heredes filios, et nepotes: et custoditur iusto substantia peccatoris.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Multi cibi in novalibus patrum: et aliis congregantur absque iudicio.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
Qui parcit virgæ, odit filium suum: qui autem diligit illum, instanter erudit.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
Iustus comedit, et replet animam suam: venter autem impiorum insaturabilis.

< Mithali 13 >