< Mithali 13 >

1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
A son wise [the] discipline of a father and a mocker not he listens to a rebuke.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
From [the] fruit of [the] mouth of a person he eats good thing[s] and [the] appetite of treacherous [people] [is] violence.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
[one who] guards Mouth his [is] protecting life his [one who] opens lips his ruin [belongs] to him.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
[is] coveting And nothing appetite his a sluggard and [the] appetite of diligent [people] it will be made fat.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
A word of falsehood he hates a righteous [person] and a wicked [person] he acts odiously and he may act shamefully.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Righteousness it preserves integrity of way and wickedness it subverts sin.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
There [is one who] enriches himself and there not [is] anything [one who] impoverishes himself and wealth great.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
[the] ransom of [the] life of A person [is] wealth his and a poor [person] not he hears a threat.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
[the] light of Righteous [people] it rejoices and [the] lamp of wicked [people] it is extinguished.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
Only with pride it gives contention and [is] with [those who] receive advice wisdom.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Wealth from vanity it will become small and [one who] gathers on hand he will increase.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Hope deferred [is] making sick [the] heart and [is] a tree of life a desire [which] comes.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
[one who] despises A word he will be pledged to it and [one] fearing a commandment he he will be rewarded.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
[the] instruction of A wise [person] [is] a fountain of life to turn aside from [the] snares of death.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Insight good it gives favor and [the] way of treacherous [people] [is] enduring.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Every sensible [person] he acts with knowledge and a fool he spreads out foolishness.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
A messenger wicked he falls in trouble and an envoy of faithfulness [is] healing.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Poverty and shame [one who] ignores discipline and [one who] keeps correction he is honored.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
A desire done is pleasing to a person and [is] an abomination of fools to turn aside from evil.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
([one who] walks *QK) With wise [people] (he will become wise *QK) and [one who] associates with fools he will be harmed.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Sinners it pursues calamity and righteous [people] it rewards good.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
A good [person] he leaves an inheritance to children of children and [is] stored up for the righteous [the] wealth of a sinner.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Abundance of food [the] unplowed ground of poor [people] and there [is what] is swept away in not justice.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
[one who] restrains Rod his [is] hating son his and [one who] loves him he seeks early him discipline.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
A righteous [person] [is] eating to [the] satiety of appetite his and [the] belly of wicked [people] it is lacking.

< Mithali 13 >